Home Makala Yanga sc Yaifuata Ruvu Kigoma

Yanga sc Yaifuata Ruvu Kigoma

by Sports Leo
0 comments

Kikosi cha klabu ya Yanga sc kimeondoka asubuhi ya leo kuelekea Kigoma kuvaana na Ruvu Shooting katika mchezo wa ligi kuu utakaofanyika katika uwanja wa Lake Tanganyika uliopo mjini Kigoma.

Mchezo huo umepelekwa mkoano humo na wenyeji wa mchezo huo ambao ni Ruvu Shooting ambapo timu mwenyeji anaruhusiwa kuchagua uwanja atakaojisikia tofauti na ule wa nyumbani katika mechi mbili za msimu mmoja  kwa mujibu wa Kanuni za ligi kuu nchini.

Mastaa Feisal Salum,Djuma Shabani,Fareed Mussa,Yannick Bangala,Jesus Moloko walionekana wakiwa uwanja wa ndege kueleka mkoani humo kusaka alama tatu muhimu katika kuhitimisha mbio za ubingwa wa ligi kuu nchini.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited