Home Makala Azam Fc Yamtema Moallin

Azam Fc Yamtema Moallin

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Azam Fc imeamua kuachana na kocha wake wa timu ya wakubwa Abdihamid Moallin pamoja na msaidizi wake Omary Nasser ambao wameachia ngazi kama kocha mkuu na msaidizi huku wakisubiri kupangiwa majukumu mengine ya kiufundi.

Maamuzi hayo yamefikiwa mapema kutokana na kutoridhishwa na mwenendo wa timu katika michezo miwili ya ligi kuu waliyocheza mpaka sasa ambapo katika michezo miwili wamefanikiwa kupata alama nne kati ya sita wakiwafunga Kagera Sugar 2-1 na kupaa sare dhidi ya Geita Gold ya 1-1.

Inasemekana kuwa mabosi wa klabu hiyo hawaridhishwi na ubora wa kikosi hicho ambapo wanaona kuwa kiwango cha timu kipo chini ukilinganisha na usajili waliofanya hivyo wanaona kama kocha hatoshi katika nafasi hiyo hivyo wanatafuta kocha mzoefu zaidi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited