Home Makala Djuma,Diarra Hatihati Kuwavaa Azam Fc

Djuma,Diarra Hatihati Kuwavaa Azam Fc

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa Klabu ya Yanga sc Nasreddine Mohamed Nabi amesema kuwa wachezaji tegemeo wa kikosi cha kwanza Djuma Shabani na Djigui Diarra wana hatihati ya kuwavaa Azam Fc katika mchezo wa ligi kuu nchini siku ya kesho kutokana na sababu mbalimbali za kiafya.

Nabi alisema hayo wakati wa mkutano na waandishi wa habari unaoandaliwa na bodi ya ligi kuu ambapo makocha huongea na waandishi wa habari za michezo siku moja kuelekea katika mchezo huo ambapo amesema kuwa Djuma alikua na Maralia siku chache zilizopita lakini ameanza mazoezi huku Diarra alikua na majeraha japo naye ameanza mazoezi hivyo kuwatumia inategemea na ripoti ya daktari.

Yanga sc na Azam Fc zitamenyana kesho katika uwanja wa Azam Complex Chamazi ambapo mara ya mwisho Yanga sc ilishinda kwa mabao 2-1 na kuondoka na alama zote tatu muhimu.

banner

Kocha wa Azam Fc Kali Ongala alisema kuwa wanajua Yanga sc iliwafunga msimu uliopita lakini sio timu hatari hivyo watajitahidi kuwatuliza mashabiki ili wapate alama tatu muhimu kwani mashabiki wa Yanga sc wamekua wanaongeza hamasa kwa wachezaji wao.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited