Home Makala Zoran Aondoka Simba sc

Zoran Aondoka Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imetangaza kuachana na kocha wake Zoran Maki ikiwa ni takribani miezi miwili tangu ajiunge na klabu hiyo kama kocha mkuu kwa mkataba wa mwaka mmoja.

Zoran ambaye ameiongoza Simba sc katika mechi rasmi moja tu ya ngao ya jamii dhidi ya Yanga sc akipoteza kwa mabao 2-1 anaondoka klabuni hapo pamoja na wasaidizi wake kocha wa viungo Sbai Karim na kocha wa makipa Mohamed Rachid ambao walijunga nae wakiwa kambini nchini Misri kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya.

Taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo zinadai kuwa kocha huyo ameomba kuondoka mwenyewe baada ya kupata ofa kutoka klabu ya Al Ittihad inayoshiriki ligi kuu nchini Misri ambapo klabu hiyo imeweka dau kubwa ambalo limewashawishi makocha hao kuondoka huku pia kukiwa na sababu zingine ambazo kocha huyo aliona ni bora kuondoka.

banner

Simba sc baada ya kuachana na Maki tayari wapo kwenye mchakato wa kutafuta kocha mwingine wa kuchukua nafasi ya Maki huku kwa sasa timu itakua chini ya uangalizi wa Seleman Matola kwa kipindi cha muda mfupi na kocha mpya atakuja mapema kuwahi michuano ya Caf ambayo Matola hana leseni hivyo hawezi kukaa benchi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited