Home Makala MVP Atua Yanga sc

MVP Atua Yanga sc

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Yanga sc imemtambulisha kiungo wao mpya raia wa Ivory Coast Pacome Zouazoua ambaye amejiunga na klabu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili kuja kusaidia mwendelezo wa kunyakua makombe klabuni hapo.

Kiungo huyo mshambuliaji ndie mchezaji bora wa ligi kuu ya soka ya Ivory Coast akiitumikia klabu ya Asec Mimosas ambapo alifunga mabao saba na kusaidia upatikanaji wa mabao mengine manne katika ligi kuu ya nchini humo.

Pacome anaungana na Stephane Aziz Ki na Koausi Yao ambao wametokea pamoja katika klabu hiyo ya Asec Mimosas ya nchini humo.

banner

Kiungo huyo ana uwezo wa kucheza vyema nafasi ya kiungo mshambuliaji na mkabaji ambapo kusajiliwa kwake kunatajwa kuwa anachukua nafasi ya kiungo Yannick Bangala ambaye nae tayari yupo katika harakati za kuondoka klabuni hapo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited