Home Makala Bangala Atua Azam Fc

Bangala Atua Azam Fc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc imefikia makubaliano na klabu ya Azam Fc juu ya kumnunua kiraka Yannick Bangala kwa dau la kiasi cha shilingi milioni 100 ambapo tayari klabu hiyo imethibitisha kuhusu dili hilo kukamilika.

Bangala alisaliwa na mkataba wa mwaka mmoja klabuni hapo ambapo tayari alishaonesha nia ya kutaka kuondoka Yanga sc ambapo klabu ilikua tayari kumuachia kwa sharti la kutojiunga na klabu yeyote kutoka Tanzania.

Baada ya vuta nikuvute ya muda mrefu hatimaye makubaliano yamefikiwa kwa pande mbili kuachana baada ya Azam Fc kuwasilisha ofa ya dau la shilingi milioni 100 na kufanikiwa kumsajili staa huyo.

banner

Bangala amekaa Yanga sc kwa misimu miwili na amefanikiwa kuchukua makombe yote ya ndani hivyo kupata changamoto mpya ndani ya klabu nyingine hapa nchini ni jambo jema kwake.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited