Home Makala Singida FG Yafungiwa Kusajili

Singida FG Yafungiwa Kusajili

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya soka ya Singida Fountain Gate Fc imefungiwa kusajili na shirikisho la soka Duniani (Fifa) mpaka itakapomlipa aliyekua mshambuliaji wa timu hiyo Nicholas Gyan baada ya kuvunja nae mkataba bila kufuata taratibu sahihi.

Klabu hiyo iliachana na mchezaji huyo ambaye mara nyingi alikua anatumika kama beki wa kulia bila kukamilisha baadhi ya malipo yake na hivyo mchezaji huyo kuamua kukimbilia kushtaki katika shirikisho la soka duniani.

banner

Fifa ilitoa siku arobaini na tano kwa Singida FG kuhakikisha imekamilisha malipo hayo lakini klabu hiyo imeshindwa kukamilisha malipo hayo kwa wakati na kusababisha kufungiwa huko kusajili wachezaji wa kimataifa.

Kutokana na adhabu hiyo kutoka Fifa nalo shirikisho la soka nchini Tanzania (TFF) limeifungia klabu hiyo kufanya usajili wa wachezaji wa ndani mpaka pale itakapokamilisha malipo ya fedha hizo kwa mchezaji huyo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited