Home Soka Kiungo Hatari Atua Simba Sc

Kiungo Hatari Atua Simba Sc

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Simba SC imekamilisha usajili wa Kiungo Babacar Sarr raia wa Senegal kama Mchezaji huru baada ya kuachana na Monastir ya Tunisia ambapo amesaini mkataba wa miaka miwili na nusu kukipiga katika klabu hiyo yenye maskani yake mitaa ya Msimbazi jijini Dar es salaam.

Kiungo huyo kabla ya kuja Simba Sc alikua anaichezea klabu ya Us Monastir ya nchini Tunisia ambapo walishiriki Arab Club Champions Cup na kucheza na Al Nassr mchezo ambao walifungwa mabao 4-1 huku staa Cristiano Ronaldo naye akicheza mchezo huo.

Simba sc imepata mtelezo kumsajili staa huyo kutokana na kuwa hana timu tangu mwezi Novemba baada ya kuachana na Us Monastry ambayo aliichezea kwa miezi sita pekee akicheza michezo saba na kufunga goli moja.

banner

Staa huyo anakuja kujibu ombi la kocha Abdelhack Benchika ambaye alikua anahitaji kiungo mkabaji baada kutoridhishwa na ufanisi wa viungo aliowakutana klabuni hapo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited