Home Soka Pamba Jiji Yaanza Kazi

Pamba Jiji Yaanza Kazi

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji Erick Okutu raia wa Ghana amejiunga na klabu ya Pamba jiji akitokea Tabora United kwa mkataba wa mwaka mmoja baada ya kumaliza mkataba na klabu yake hiyo ya zamani iliyompokea nchini msimu uliopita.

Erick alifanikiwa kufunga mabao 7 msimu uliopita akiwa chini ya kocha Goran Kopunovic ambaye kwa sasa ni kocha wa Pamba Jiji baada ya kuondoka Tabora United akijiuzuru nafasi yake ya ukocha mkuu kutokana na masuala ya malipo kutokua sawa.

Tayari kocha huyp yupo jijini Mwanza na ameshaanza kutoa mapendekezo yake juu ya usajili wa mastaa wapya klabuni hapo ikiwemo usajili wa winga huyo msumbufu.

banner

Pamba imeachana na karibia kikosi kizima kilichoipandisha daraja msimu uliopita huku wachache wanaohitajika wakipewa mikataba kimya kimya ya kusalia klabuni hapo ambapo wataungana na mastaa wapya kuunda jezi la kuutetea mkoa wa Mwanza katika ligi kuu nchini.

Mbali na Okuta kikosi hicho mpaka sasa kimeshawatambulisha Yona Amos,Samson Madeleke,Benny Nakibinde,Salehe Masoud,Ibrahim Abdallah,Justine Omary Billal na Frank Ng’amba.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited