Ni kama zali la mentali kwa mshambuliaji Ibrahimu Ajibu baada ya kusota akiwa jangwani na sasa anakula raha katika hoteli aliyokaa staa wa Uingereza Wayne Rooney akiwa na mastaa wenzake wa Simba sc.
Iko hivi,Simba imeweka kambi nchini Afrika ya kusini kujiandaa na msimu mpya wa ligi kuu na michuano ya kimataifa na kambi hiyo imewekwa katika mji wa Rustenburg ulioko kaskazini magharibi mwa nchi hiyo ambapo katika hoteli waliyofikia mastaa wa klabu hiyo ni hoteli ambayo ilitumiwa na mastaa wa timu ya taifa ya Uingereza katika fainali za kombe la dunia 2010 nchini humo.