Home Makala TFF Yapiga Nyundo Viwanja Vitatu

TFF Yapiga Nyundo Viwanja Vitatu

by Dennis Msotwa
0 comments

Shirikisho la soka nchini imeamua kuvifungia viwanja vya CCM Kirumba,Jamhuri Pamoja na CCM Liti uliopo mjini Singida kutokana na kuwa na miundombinu iliyochakaa kwa mujibu wa kanuni na leseni za ligi kuu nchini kuhusu viwanja vya michezo ya ligi kuu ya Nbc.

Taarifa za kufungiwa kwa viwanja hivyo vinavyotumiwa na timu za Pamba Jiji,Singida Black Stars Pamoja na Dodoma jiji Fc ambapo sasa vilabu hivyo vinapaswa kutafuta viwanja vingine kwa ajili ya michezo yao ya ligi kuu.

banner

Taarifa iliyotolewa na Shirikisho la soka nchini (TFF) imesema kuwa miundmbinu ya viwanja hivyo haijakidhi matakwa ya kanuni kama ilivyoainishwa kwenye masharti ya Kanuni na leseni za klabu za ligi kuu ya Nbc nchini.

Timu za Singida Black Stars,Pamba Jiji Fc,Dodoma Jiji Pamoja na Tabora United sasa zinapaswa kutafuta viwanja vingine kwa ajili ya michezo yao ya nyumbani.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited