Home Makala Azam Fc Yaifuata Singida Black Stars

Azam Fc Yaifuata Singida Black Stars

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Azam Fc imeanza safari mapema ya leo kuifuata Singida Black Stars katika mchezo wa ligi kuu ya Nbc nchini utakaofanyika kesho jumapili katika uwanja wa Ccm Liti mjini Singida.

Azam Fc baada ya kushinda 3-0 dhidi ya Kengold Fc ilirejea Dar es Salaam na leo alfajiri imeanza safari kwa kutumia treni ya mwendokasi mpaka dodoma kisha itapanda basi moja kwa moja mpaka Singida.

banner

Kocha Rachid Taoussi anatarajiwa kuingiza kikosi chake kamili katika mchezo huo kutokana na kuhitaji kupata nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa ambapo Singida Black Stars ni washindani wakubwa wa nafasi hiyo.

Punde baada ya kupata ushindi dhidi ya Kengold Fc kocha alisema kuwa anahitaji pia kushinda michezo inayofuatia.

“Vijana wanapambana, morali ya ushindi wanayo, lakini hii ni kutokana na ubora na uimara wa timu, niwapongeze lakini tunaenda kujipanga na mechi zinazofuata,” amesema kocha huyo.

Katika msimamo wa ligi kuu mpaka sasa Azam Fc wapo nafasi ya tatu na alama 51 katika michezo 24 huku Singida Black Stars wakiwa nafasi ya nne na alama 47 katika michezo 24.

 

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited