Home Makala Sowah Kujiunga Simba Sc

Sowah Kujiunga Simba Sc

by Dennis Msotwa
0 comments
Sowah Kujiunga Simba Sc;Sportsleo.co.tz

Klabu ya Simba Sc imefanikiwa kufikia makubaliano na klabu ya Singida Black Stars juu ya usajili wa mshambuliaji Jonathan Sowah ambaye sasa atajiunga na klabu hiyo yenye makao yake makuu Msimbazi jijini Dar es Salaam.

Awali Singida Black Stars ilidai kuwa timu yeyote inayomhitaji mshambuliaji huyo inapaswa kulipa shilingi bilioni moja ili kuvunja mkataba wake uliosalia klabuni hapo.

Taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo ya Singida Black Stars imesema kuwa dili hilo limekamilika kutokana na Rais wa heshima wa Singida Black Stars kuamua kumtoa mshambuliaji huyo kwa makubaliano maalumu na Rais wa heshima wa klabu ya Simba Sc Mohammed Dewji.

banner

Baada ya makubaliano baina ya mabosi hao wa juu wa klabu hizo moja kwa moja klabu ya Simba Sc ilipewa ruhusa ya kuzungumza kuhusu maslahi binafsi ambapo walifikia makubaliano na sasa staa huyo moja kwa moja atajiunga na kambi ya Simba Sc moja kwa moja nchini Misri.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited