Home Makala MO Dewji Ajiuzuru Simba.

MO Dewji Ajiuzuru Simba.

by Dennis Msotwa
0 comments

Mwenyekiti wa bodi ya Simba Mohammed Dewji ametangaza kujiuzuru nafasi yake katika bodi na kubaki kama mwekezaji.

Hii ni baada ya Simba kushindwa kuchukua Kombe la Mapinduzi kwa kufungwa na Mtibwa Sugar bao 1-0 na vijana hao kunyakua ubingwa katika uwanja wa Amani visiwani Zanzibar.

“Ni huruma Simba hawajaweza kushinda mchezo huu baada ya kuwalipa mishahara ya karibu bilioni 4 kwa mwaka ,hivyo najiuzuru kama mwenyekiti wa bodi na nitabaki kama mwekezaji Simba nguvu moja nitazingatia kukuza miundombinu na taaluma ya vijana “Alisema Mohammed Dewji.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited