Kaimu kocha mkuu wa Yanga Boniface Mkwasa amesema kuwa kwa sasa hajui hatma yake tangu nafasi ya Mwinyi Zahera kuchukuliwa na Mbelgiji Luc Eymael.
Tumefurahi ujio wa kocha mpya ndani ya Yanga na tunatoa ushirikiano wa kutosha kuhakikisha anafanya kazi vizuri kwa kumuelekeza utaratibu wote wa timu.
“Kwa upande wangu bado sijajua hatma yangu viongozi ndio wanaojua na ndio wenye majibu kuhusu uwepo wangu ndani ya timu ,kwa sasa bado naendelea kukinoa kikosi hadi kocha mpya atakapokabidhiwa rasmi kikosi”alisema Boniface Mkwasa.