Home Soka Molinga Aponea ChupuChupu

Molinga Aponea ChupuChupu

by Dennis Msotwa
0 comments

Ni kama zali la mentali baada ya mshambuliaji wa Yanga David Molinga kuponea chupuchupu kutemwa baada ya kurejeshwa kikosini dakika za mwisho wakati wa dirisha la usajili lililofungwa wiki hii.

Iko Hivi,baada ya kuja kwa kocha mpya Luc Aymael ambaye aliangalia video za mechi zilizopita na kuuliza alipo mshambualiaji huyo mwenye mabao 5 katika timu hiyo na kujibiwa ameachwa kutokana na matatizo ya kinidhamu ndipo alipoagiza mchezaji huyo arejeshwe kikosini haraka.

Kwa mujibu wa Aymael,Mchezaji huyo ameona ana msaada katika timu hiyo kufuatia aina ya uchezaji wa staa huyo kuona unaweza kuisaidia timu hiyo hivyo kumrejesha haraka kuungana na timu.

banner

Yanga imewatema wachezaji kadhaa hasa mastaa iliyowasajili msimu uliopita kama Juma Balinya,Sadney Urikhob,Mustapha Selemani,Mybin Kalengo na Issa Bigirimana huku ikiwatoa kwa mkopo Ali Hamad Ali,Rafael Daud na Cleofasi Sospeter.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited