Home Makala Tukikutaka Hatukukosi

Tukikutaka Hatukukosi

by Sports Leo
0 comments

Imezoeleka kwa vilabu vya hapa nchini, havisajili wachezaji wenye mikataba, mara nyingi husubiri mikataba ifike mwisho kisha kusajili wachezaji walio huru

Hata hivyo Yanga kupitia wadhamini/wahisani wao GSM, usajili wa kuelekea msimu ujao watafanya mambo tofauti

Imeelezwa GSM walimpa mkufunzi wa Yanga Luc Eymael uhuru wa kupendekeza wachezaji anaotaka wasajiliwe bila ya kujali kama mikataba yao inamalizika mwishoni mwa msimu au la

banner

Mabilionea hao wamejipanga kutumia ‘fedhwa’ kufanya usajili wa maana na pengine kwa mara ya kwanza kwenye usajili ujao wa Yanga inaweza kushuhudiwa mchezaji akanunuliwa hata kwa Tsh Milioni 500 au zaidi ili mradi tu awe na sifa na pia awe amehitajika na kocha

Na ndio maana pamoja na kufahamu mshambuliaji Heritier Makambo kuwa na mkataba Horoya AC, klabu ya Yanga imeanza mazungumzo na klabu hiyo ili kuipa sahihi ya nyota huyo aliyejitengenezea jina licha ya kuitumikia Yanga kwa msimu mmoja tu

Jana Mkurugenzi wa Uwekezaji GSM Mhandisi Hersi Said alisema kampuni hiyo itashirikiana na uongozi wa Yanga kufanya usajili kabambe ambao wana uhakika utawapa ubingwa msimu ujao

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited