Home Soka Kocha Simba Amkomalia Ndemla

Kocha Simba Amkomalia Ndemla

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa klabu ya Simba Sven Vandebroek amesema bado anamhitaji kiungo Said Ndemla katika klabu hiyo licha ya kumuweka benchi katika michezo mbalimbali.

Kocha huyo raia wa Uholanzi amesema hayo wakati akijibu maswali ya mashabiki kupitia mitandao ya kijamii ya klabu hiyo ambapo alisema “Ndemla ni mchezaji mzuri anayetumia mguu wa kulia huku akipiga pasi ndefu na fupi zinazofika japo anabanwa na changamoto ya kutokua na nguvu”.

Kocha huyo alisisitiza kumhitaji Ndemla kwa kua kila anahitaji kila eneo liwe na wachezaji bora huku akifurahishwa na hatua ya kiungo huyo kutoshuka kiwango licha ya kukaa benchi mara kwa mara.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited