Home Makala Diogo Jota Anukia Lazio

Diogo Jota Anukia Lazio

by Dennis Msotwa
0 comments

Lazio ina mpango wa kuimarisha kikosi msimu ujao kwa kumnyakua staika wa Wolverhampton Wanders,Diogo Jota ambaye ni mchezaji wa kimataifa wa Ureno .

Nyota huyo anaweza kujiunga na klabu hiyo ya Serie A endapo Biancoceleste kama inavyofahamika itafuzu kucheza ligi ya mabingwa Ulaya msimu ujao.

Jota kwa sasa ana umri wa miaka 23 pia ana mkataba na Wolves unaomalizika June 2022 huku tayari akiwa amefunga mabao 6 na kutengeneza pasi 7 katika mechi 25 za ligi.

banner

Msimu uliopita Lazio iliwauzia Wolves wachezaji wawili kutoka Ureno ,Pedro Neto na Bruno Jordao hivyo kutokana na uhusiano wao wa karibu na wakala wa Jota,Jorge Mendes unaweza ukarahisisha dili hilo.

Lazio kwa sasa ipo nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi ikizidiwa pointi moja na Juventus kabla ya msimu kusimamishwa kutokana na kupambana na virusi vya Corona.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited