Home Makala Nilichuniwa Siku Tatu-Pulisic

Nilichuniwa Siku Tatu-Pulisic

by Dennis Msotwa
0 comments

Cristian Pulisic mwenye miaka 21 anayekipiga kwenye klabu ya Chelsea akitokea ndani ya Borussia Dortmund amesema kuwa siku ya kwanza wachezaji wenzake walimchunia ndani ya gari walipokuwa njiani kuelekea mazoezini.

Nyota huyo aliyesajiliwa majira ya joto aliongeza kuwa hakuna aliyetaka kumfahamu, kumsemesha wala kumtakia kila la kheri kwenye maisha yake mapya jambo lililomfanya ajiulize mara mbili yupo sehemu gani.

“Siku tatu za mwanzo hakuna mchezaji aliyekuwa akinijali kila mtu aliniona ni mtu wa kawaida ila nilipoanza kufunga na kutoa pasi za mabao wakaanza kunipa ushirikiano,” alisema Pulisic

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited