Home Soka Niyonzima Yupo Sana Jangwani

Niyonzima Yupo Sana Jangwani

by Dennis Msotwa
0 comments

Kiungo Maestro wa klabu ya Yanga sc Haruna Niyonzima amesaini mkataba mpya wa kuendelea kusalia katika klabu hiyo yenye maskani yake mitaa ya Jangwani na Twiga Kariakoo baada ya ule wa awali kuelekea mwishoni.

Kuongeza mkataba kwa kiungo huyo kumetokana na mapendekezo ya kocha Cedrick Kaze kuhitaji kiungo huyo asalie kikosini licha ya kutokua na uhakika wa kuanza mara kwa mara kikosi cha kwanza.

“Tupo vizuri kwa ajili ya kufanya usajili ambao ni pendekezo la mwalimu, ripoti ipo tayari na tutaitumia katika kuboresha kikosi ili kiwe bora.
“Wapo wachezaji ambao wataongeza mkataba ndani ya timu, wengine wataondolewa kwa mkopo pia wapo ambao wataongezwa ndani ya timu.
“Tayari tumekamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji Saido Ntibanzokiza ambaye yeye kila kitu kimekamilika kilichobaki kwa sasa ni mwalimu mwenyewe kuamua kumtumia akiona inafaa,” . Alisema Eng.Hersi ambaye ndie mkurugenzi wa uwekezaji kampuni ya Gsm inayoifadhili na kuidhamini klabu ya Yanga sc.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited