Home Soka Ulimwengu Aibeba Tp Mazembe

Ulimwengu Aibeba Tp Mazembe

by Dennis Msotwa
0 comments

Mshambuliaji Thomas Ulimwengu Januari 6 aliisaidia TP Mazembe ya Congo kushinda mabao 2-1 dhidi ya Bouenguidi ambapo alikuwa miongoni mwa washambuliaji waliopeleka kilio kwa wapinzani hao mapema.

Ushindi huo uliopata klabu hiyo unamaanisha kwamba imefuzu hatua ya makundi ya klabu bingwa barani Afrika ambapo dakika ya 14 alipachika bao la kuongoza ambalo liliwapa nguvu Mazembe na baadae walipachika bao la pili dakika ya 45 na kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 2-0 wakiwa Uwanja wa Stade TP Mazembe.

Mpaka mpira unaisha Bouenguidi walikubali kipigo hicho huku wakipata bao la kufutia machozi dakika ya 79 kupitia kwa Djoe Dayan Boussougou ila halikuweza kuwapa faida wapinzani hao kusong mbele hivyo watashiriki Kombe la Shirikisho.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited