Inawezekana mshambuliaji John Bocco akawakosa Zambia katika mchezo wa kundi D kwenye michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (Chan) yanayoendelea nchini Cameroon.
Nahodha huyo wa timu ya taifa ya Tanzania iliyoko katika michuano hiyo anatajwa kutokuwa fiti bado na yawezekana Erasto Nyoni akavaa kitambaa cha unahodha badala yake katika mchezo utaopigwa uwanja wa Limbe, saa 1:00 Usiku ( EAT ).