Home Makala Yacouba Arejea Yanga sc

Yacouba Arejea Yanga sc

by Dennis Msotwa
0 comments

Mshambuliaji Yacouba Songne amepona na Sasa yuko fiti kuanza kukitumikia kikosi cha Timu ya Wananchi kuanzia michezo ijayo.

Daktari wa timu, Nahumu Muganda amesema pamoja na Yacouba, beki Abdallah Shaibu ‘Ninja’ na kipa Ramadhan Kabwili nao wamepona na wamerejea kikosi.

“Yacouba tayari ameshapona na ameshaanza mazoezi na timu, tutakaporejea kambini kesho atakuwa tayari kutumika kadri Kocha atakavyoona inafaa kikosini,” amesema Dkt. Muganda.

banner

Amesema Ninja na Kabwili pia wameshapona na wameanza mazoezi ya pamoja timu na wao wako tayari kutumika hivyo kuingiza idadi ya majeruhi kwenye kikosi.

“Tulikuwa na majeruhi saba, ukijumusia Mukoko lakini Mukoko naye yuko sawa na amenieleza kwamba kesho atarudi kambini na wenzake, hivyo tutabaki na majeruhi watatu ambao ni Said Ntibazonkiza, Dickson Job na Balama Mapinduzi,” Amesema Dkt. Muganda.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited