Kocha Juma Mwambusi ameanza kutekeleza programu yake ya mazoezi leo kwa kuanza na dozi nene ya asubuhi na jioni kwa wachezaji wake.
Mara baada ya kukabidhiwa mikoba rasmi Kocha Mwambusi amewasilisha programu yake ambayo kwa siku Nne za mwanzo vijana watafanya mazoezi mara mbili kisha Ijumaa watafanya mara moja.
“Programu hii imelenga kurejesha utimamu wa mwili kwa wachezaji lakini pia kujenga uwezo wa pamoja kama timu kutokana na mapungufu ambayo yalionekana kwenye kikosi,” amesema Kocha Mwambusi.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Amesema anaamini kikosi kitakaa sawa muda si mrefu na baada ya wiki hii ataangalia ratiba kama itaruhusu mchezo wa ndani wa kujipima mguvu.