Home Soka Tizi La Mwambusi Usipime

Tizi La Mwambusi Usipime

by Dennis Msotwa
0 comments

Kocha Juma Mwambusi ameanza kutekeleza programu yake ya mazoezi leo kwa kuanza na dozi nene ya asubuhi na jioni kwa wachezaji wake.

Mara baada ya kukabidhiwa mikoba rasmi Kocha Mwambusi amewasilisha programu yake ambayo kwa siku Nne za mwanzo vijana watafanya mazoezi mara mbili kisha Ijumaa watafanya mara moja.

“Programu hii imelenga kurejesha utimamu wa mwili kwa wachezaji lakini pia kujenga uwezo wa pamoja kama timu kutokana na mapungufu ambayo yalionekana kwenye kikosi,” amesema Kocha Mwambusi.

banner

Amesema anaamini kikosi kitakaa sawa muda si mrefu na baada ya wiki hii ataangalia ratiba kama itaruhusu mchezo wa ndani wa kujipima mguvu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited