Home Soka Kante Aizibia Real Madrid

Kante Aizibia Real Madrid

by Sports Leo
0 comments

Kiungo Ngolo Kante alikua kikwazo kwa Real Madrid kuibuka na ushindi mbele ya Chelsea katika mchezo wa nusu fainali klabu bingwa barani ulaya uliofanyika nchini Hispania.

Kiungo huyo aliwadhibiti ipasavyo viungo wa Real Madrid wakiongwa na Ton Kroos na Casemiro kiasi cha kushindwa kuipeleka timu juu na kusababisha bao la uongozi kwa Chelsea kupitia kwa Christian Pullisic dakika ya 14 huku Madrid wakisawazisha robo saa baadae kwa kiki ya Karim Benzema kufuatia pasi ya Elder Militao.

Kazi kubwa iliyofanywa na Kante ilimfanya Pullisic kuwa huru muda nwingi kiasi cha kuweka rekodi ya kuwa Mmarekani wa kwanza kufunga goli hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo huku Madrid wakipiga mashuti machache zaidi yaliyolenga lango tangu msimu wa 2003-2004.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited