Kiungo wa klabu ya Yanga sc Serge Mukoko Tomombe ameitwa katika kikosi cha wachezaji 32 kuelekea katika mechi ya kirafiki dhidi ya Tunisia itakayofanyika juni 10 nchini Tunisia.
Hii ni mara ya pili kwa kiungo huyo kuitwa ambapo mara ya kwanza alifanikiwa kuitumika timu hiyo jumla ya dakika 135 katika michezo ya kirafiki na kimashindano.
Mukoko atakua na kazi ya kugombania namba mbele ya mastaa mbalimbali wanaocheza eneo la kiungo akiwemo Gael Kakuta na wengineo kama Mika Michee, Fabrice Ngoma, Mercey Ngimbi, Paul-Jose Mpoku, Yannick Bangala na Mpanzu Pelly.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.