Home Soka Mukoko Kumfuata Makambo Horoya Fc

Mukoko Kumfuata Makambo Horoya Fc

by Sports Leo
0 comments

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Guinea ni kwamba klabu ya Horoya inataka kumnunua kiungo mkabaji wa klabu ya Yanga sc, Mukoko Tonombe na wamejiandaa kuwasilisha Ofa kubwa mezani kwa klabu hiyo ambao ni mabingwa wa ligi kuu mara 27.

Ripoti zinaeleza kuwa Horoya wamejipanga kumsajili Mukoko kwa dau la uhamisho wa dola 200,000 (TSh. 464 milioni) na mshahara mnono wa dola 9000 (Tsh. 18 milioni) kwa mwezi  ambao ni takribani mara tatu ya stahiki anazopewa na klabu yake kwa sasa.

Ikumbukwe kiungo huyo amebakiza mwaka mmoja katika mkataba wake na Yanga sc ambapo ilimsainisha mkataba wa miaka miwili ikimnunua kutoka klabu ya As Vita msimu ulioisha.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited