Home Soka Messi avunja rekodi ya Pele

Messi avunja rekodi ya Pele

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa Argentina Lionel hatimaye amevunja rekodi ya ufungaji wa mabao Amerika ya Kusini iliyokuwa ikishikiliwa  na gwiji wa soka duniani kutoka Brazil Pele mwenye mabao 77 kwa muda mrefu.

Messi amefikia na kuvunja rekodi hiyo usiku wa kuamkia leo alipoifungia timu yake ya taifa ya Argentina mabao matatu (hat-trick) katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Bolivia kwenye mechi ya kufuzu kombe la dunia Qatar 2022.

Kabla ya mchezo huo La purga alikuwa na mabao 75 mawili nyuma ya Pele lakini baada ya kupiga hat-trick amevunja rekodi hiyo na kufikisha mabao 78 na kuwa kinara.

banner

Argentina ipo nafasi ya pili katika msimamo wa kufuzu kombe la dunia wakiwa na pointi 18 nyuma ya Brazil wanaoongoza wakiwa na pointi 24.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited