Home Soka Kiiza kutua Kagera

Kiiza kutua Kagera

by Dennis Msotwa
0 comments

Mshambuliaji wa zamani wa vilabu vya Yanga na Simba Hamisi Kiiza ‘Diego’ yuko mbioni kutua nchini kujiunga na watengeneza sukari Kagera Sugar kwenye dirisha hili dogo la usajili.

Mchezaji huyo aliwahi kufanya vizuri nchini katika klabu ya Yanga na kufanikiwa kutwaa mataji ya ligi kuu soka nchini pia atakumbukwa kwa mchango wake katika kupachika mabao kulikoiwezesha timu hiyo kutwaa ubingwa Afrika Mashariki na Kati(CECAFA) mwaka 2014 kwa kufunga mabao 5 kwenye michuano hiyo.

Kiiza alihudumu Yanga kuanzia mwaka 2011 hadi mwak 2015 kabla ya kujiunga na wapinzani wao wa jadi Simba mwaka 2015 hadi 2016.

banner

Kagera wanashikilia mkia kwenye msimamo wa ligi kuu ya NBC huku tatizo kubwa likiwa ni kushindwa kufunga magoli ya kutosha kufuatia kuondoka kwa washambuliaji wake Vitalis Mayanja na Yusuph Mhilu waliokuwa tegemezi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited