Home Makala Moloko Apigwa Kisu

Moloko Apigwa Kisu

by Dennis Msotwa
0 comments

Winga wa klabu ya Yanga sc Jesus Moloko Ducapel amefanyiwa upasuaji mdogo wa goti la kulia kutokana na kupata majeraha siku kadhaa zilizopita katika mchezo wa kombe la shirikisho dhidi ya Biashara United na kutolewa nje kipindi cha kwanza.

Moloko mwenye mchango mkubwa katika kikosi cha Yanga akichangia kwa mabao 3 na pasi za mwisho 3 atakua nje ya uwanja kwa kipindi kifupi kwa mujibu wa taarifa kutoka klabuni hapo.

Nafasi ya winga huyo mwenye nguvu itakwenda kuzibwa na Dennis Nkane pamoja na Chico ushindi ambaye amerejea kutoka katika majeraha huku winga Deus Kaseke nae akileta upinzani kuwania nafasi hiyo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited