Home Makala Arteta Anaamini Kubaki Kwa Auba Emirates

Arteta Anaamini Kubaki Kwa Auba Emirates

by Sports Leo
0 comments

Kocha mkuu wa Arsenal,Mikel Arteta anaamini kuwa mshambuliaji wake namba moja Pierre Emerick Aubameyang atasaini dili jipya Emirates kwani hii ni timu yake bora na wakiwa pamoja watafanya mambo makubwa.

Arteta ameongoza kikosi chake kutwaa mataji mawili mfululizo ikiwa ni pamoja na ule wa Kombe la FA ambapo aliichapa Chelsea mabao 2-1 na taji la ngao ya jamii kwa ushindi wa penalti 5-4 mbele ya Liverpool baada ya dakika 90 kutoka sare ya bao 1-1.

Aubameyang ndiye aliyefanikisha kutwaliwa kwa mataji hayo baada ya kufunga mabao 3 pekee kwenye michezo yote miwili,moja ikiwa ni lile la sare na Liverpool na mawili aliyowapa kichapo Chelsea kwenye kombe la FA.

banner

Msimu mpya wa ligi kuu England unatarajiwa kuanza Septemba 12 na mabingwa watetezi wakiwa ni Liverpool wenye uwanja wao maarufu kama Anfield.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited