Katika mchezo wa ligi kuu bara leo uliochezwa mkoani Morogoro uwanja wa Gairo umewapandisha nafasi ya 13 Mtibwa Sugar wakiwa na pointi 41 baada ya kuwafunga Azam Fc bao 1-0.
Bao hilo la kona lilifungwa na beki wa kushoto wa Mtibwa Sugar ,Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ dakika ya 37.
Mtibwa Sugar wameweza kulilinda bao hilo la pekee hadi dakika 90 za mchezo zilipotimilika kwani walifanyiwa mashambulizi mengi ya hatari ila umahiri wao wa ulinzi ukiongozwa na kipa chipukizi, Aboutwalib Mshery ndio uliyowafanya kunyakua alama tatu dhidi ya Azam Fc.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Azam Fc baada ya kupoteza mchezo huu wa leo wamebaki nafasi ya pili katika mchezo wa 35 wakiwa na pointi 65.