Home Makala Azam Fc Kujipima Dhidi Ya KMC Leo

Azam Fc Kujipima Dhidi Ya KMC Leo

by Sports Leo
0 comments

Azam Fc iliyochini ya kocha mkuu Arstica Cioaba ambaye pia ni raia wa Romania inatarajia kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya KMC leo majira ya saa 1:00 usiku katika uwanja wao uliopo Chamazi,Azam Complex.

KMC ilikuwa na mchezo wa kirafiki jana na Simba Sc Uwanja wa Uhuru ambapo ilipoteza kwa kufungwa mabao 3-1 hivyo leo watacheza mchezo wa pili na Azam Fc ambao waliwapiga mabao 2-1 Namungo Fc kwenye mchezo wa kirafiki siku ya Azam Festival.

Lengo la mchezo wa leo ni kujiweka sawa kwa ajili ya ligi kuu bara inayotarajiwa kuanza Septemba 6 ambapo Azam Fc watafungua pazia na klabu ya Polisi Tanzania.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited