Home Makala Azam Fc Yaipiga Mkwara Simba

Azam Fc Yaipiga Mkwara Simba

by Sports Leo
0 comments

Katika maandalizi kuelekea mechi dhidi ya Simba sc katika mchezo wa ngao ya hisani Azam imeifunga Namungo mabao 8-0 katika mchezo uliofanyika uwanja wa chamazi complex hapo jana.

Azam ambao pia wanakabiliwa na mechi ya marudiano dhidi ya Fasil Kanema katika kombe la shirikisho itawavaa wanamsimbazi ambao waliwafunga goli tatu katika mchezo wa ligi kuu msimu uliopita huku Meddie Kagere akifunga mabao mawili katika mechi hiyo.

Mabao ya Azam dhidi ya timu hiyo iliyopanda daraja yalifungwa na Djodi,Seleman,Sure Boy,Kangwa,Chilunda,Chirwa,Kassim na Idd Kipagwile alihitimisha karamu hiyo ya mabao kwa penati.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited