Home Makala Azam Fc Yamsajili Chilambo

Azam Fc Yamsajili Chilambo

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya soka ya Azam Fc imefanikiwa kukamilisha usajili wa beki wa kulia wa klabu ya Ruvu Shooting Nathaniel Chilambo kwa mkataba wa miaka miwili ikiwapiku klabu ya Simba sc iliyokua inamnyemelea staa huyo kinda.

Azam Fc tayari wamemsainisha mkataba wa awali staa huyo ambaye alishakubaliana maslahi binafsi na klabu ya Simba sc ambapo alikubali dau la usajili kiasi cha shilingi milioni 30 za kitanzania na mshahara wa milioni 2 kwa mwezi ambapo amelazimika kusaini Azam Fc baada ya timu hiyo kumpa maslahi bora zaidi ya hayo.

Simba sc ilikua inahitaji beki wa kulia kumpa changamoto Shomari Kapombe huku katika ripoti za usajili jina la beki huyo lilikuwepo na sasa watalazimika kuangalia mbadala mwingine.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited