Home Makala Azam Fc,Mazembe Hakuna Mbabe

Azam Fc,Mazembe Hakuna Mbabe

by Sports Leo
0 comments

Mchezo wa kirafiki baina ya Azam Fc na Tp Mazembe umemalizika kwa sare ya 1-1 baada ya dakika 90 za mchezo huo uliofanyika katika uwanja wa Ndola nchini Zambia.

Mchezo huo wa kimataifa wa kirafiki ambao Azam Fc walialikwa na Tp Mazembe ulikua wa kasi na kosa kosa nyingi huku ukiwa na ufundi wa hali ya juu ambapo Azam Fc iliandika bao la kwanza na pekee katika mchezo huo dakika ya 36 likifungwa na Kipre Junior baada ya mpira kushinda kipa wa Mazembe.

Hata hivyo bao hilo lilidumu kwa dakika 20 pekee ambapo dakika ya 57 Zemanga Soze aliisawazishia Tp Mazembe kwa shuti kali baada ya mpira kuzagaa nje ya eneo la 18 la Azam Fc.

banner

Azam Fc imepata kipimo sahihi kuelekea raundi ya pili ya michuano ya kimataifa ambapo ilipata bahata ya kuanzia katika raundi hiyo huku Simba na Yanga sc pamoja na Geita Gold Fc zilianzia raundi ya awali ya michuano ya kimataifa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited