Home Makala Azam Yacheza Na Rada Za Yanga

Azam Yacheza Na Rada Za Yanga

by Dennis Msotwa
0 comments

Wakati Yanga Sc ipo kwenye anga ya kufanya maboresho ya kikosi chake ili kuwa na ushindani kwenye namba zote kuanzia kipa mpaka wachezaji wa ndani, vita yao sasa inaongezewa makali na Azam Fc ambao wameshapaki basi lao ndani ya Kagera Sugar wakianza na Awesu Awesu ambaye ni kiungo aliyekuwa pia kwenye rada za Yanga.

Mabosi wa Yanga wapo kwenye jitihada za kumvutia kasi kipa namba moja wa Kagera Sugar, Benedickt Tinoco ili aongeze nguvu katika kikosi chao msimu ujao kwani hawakuwa na msimu mzuri ndani ya 2019/20.

Antonio Nugaz ambaye ni ofisa uhamasishaji wa Yanga amesema kuwa Tinoco wa Kagera Sugar ni kipa mwenye uwezo mkubwa na anakubalika hivyo anaweza kuibukia Yanga siku ya Mwanachi akaendeleze kutoa changamoto kwa Metacha Mnata, Faroukh Shikhalo na Ramadhan Kabwili.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited