Home Makala Baleke Hatari Tupu

Baleke Hatari Tupu

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa klabu ya Simba sc Jean Baleke amedhihirisha umahiri wake katika kuzifumania nyavu baada ya kufunga mabao matatu katika ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa ligi kuu nchini uliofanyika katika uwanja wa Manungu mkoani Morogoro.

Iliwachukua Simba sc dakika 3 pekee kupata bao la uongozi likifungwa na Baleke baada ya kumzidi maarifa beki wa Mtibwa Sugar huku pia akifungwa mengine dakika za 7 na 34 kwa nzuri ya viungo washambuliaji wa klabu hiyo wakiongozwa na Saido Ntbanzokiza na Cletous Chama.

Simba sc sasa imefikisha jumla ya alama 57 katika michezo 24 ya ligi kuu nchini huku ikiwa katika nafasi ya pili ya msimamo wa ligi hiyo na ikikabiliwa na kibarua kigumu cha kuvaana na Ihefu Fc mchezo unaofuata wa ligi kuu ugenini mkoani Mbeya.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited