Home Makala Balozi Bana Aitembelea Simba sc

Balozi Bana Aitembelea Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Ikiwa nchini Nigeria katika kujiandaa na mchezo wa hatua ya awali dhidi ya Plateau United ya nchini humo,Klabu ya Simba sc imetembelewa na Balozi wa Tanzania nchini humo Dk.Benson Bana katika kambi ya timu jijini Abuja.

Taarifa iliyochapishwa katika ukurasa wa mitandao ya kijamii ya klabu hiyo ilionyesha kwamba Balozi huyo alitembelea kambi hiyo na kukutana na wachezaji na viongozi pamoja na kukabidhiwa jezi ya klabu hiyo.

”Balozi wa Tanzania nchini Nigeria, Dkt. Benson Bana ametembelea kambi yetu hapa jijini Abuja ambapo amepata nafasi ya kuzungumza na viongozi na wachezaji na pia kukabidhiwa zawadi ya jezi mpya ambayo tutaitumia kwenye Ligi”Ilisomeka taarifa hiyo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited