Klabu ya Dodoma Jiji Fc imekamilisha usajili wa kiungo Randy Bangala Litombo kutoka nchini Congo Drc ambaye anakuja kuongeza nguvu katika eneo la katikati mwa uwanja wa timu hiyo.
Viongozi wa Dodoma Jiji Fc wameshawishika kumsajili Randy baada ya kuvutiwa na kiwango chake alipokua akiichezea timu ya Insta United kwenye michuano ya Ndondo Cup ambapo pia timu ya Polisi Tanzania ilikua ikiwania saini ya mchezaji huyo.
Dodoma jiji imekua na msimu mzuri tangu ipande ligi kuu tofauti na klabu zingine ambazo zikipanda daraja zimeshindwa kudumu katika fomu zao na kusababisha kukaa msimu mmoja na kushuka daraja ama kuponea kwenye play Off.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Bangala ambaye ni ndugu na kiungo wa Yanga sc Yannick Bangala tayari ameshajiunga na kambi ya mazoezi ya klabu hiyo jijini Dodoma.