Home Makala Bangala Atua Dodoma Jiji

Bangala Atua Dodoma Jiji

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Dodoma Jiji Fc imekamilisha usajili wa kiungo Randy Bangala Litombo kutoka nchini Congo Drc ambaye anakuja kuongeza nguvu katika eneo la katikati mwa uwanja wa timu hiyo.

Viongozi wa Dodoma Jiji Fc wameshawishika kumsajili Randy baada ya kuvutiwa na kiwango chake alipokua akiichezea timu ya Insta United kwenye michuano ya Ndondo Cup ambapo pia timu ya Polisi Tanzania ilikua ikiwania saini ya mchezaji huyo.

Dodoma jiji imekua na msimu mzuri tangu ipande ligi kuu tofauti na klabu zingine ambazo zikipanda daraja zimeshindwa kudumu katika fomu zao na kusababisha kukaa msimu mmoja na kushuka daraja ama kuponea kwenye play Off.

banner

Bangala ambaye ni ndugu na kiungo wa Yanga sc Yannick Bangala tayari ameshajiunga na kambi ya mazoezi ya klabu hiyo jijini Dodoma.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited