Home Makala Bongo Waomba Ligi Kuu Iahirishwe

Bongo Waomba Ligi Kuu Iahirishwe

by Sports Leo
0 comments

Timu ya Arusha FC inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza kupitia Ofisa habari wake Bahati Msilu wameliomba Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kufuta msimu wa Ligi Daraja la Kwanza 2019/20 kutokana na janga la Virusi vya Corona linaloendelea kuitikisa Dunia.

Msilu alisema hayo baada ya kuona mapumziko ya kujikinga na ugonjwa wa Covid-19 yameharibia utaratibu wote kwa kusababishia gharama zisizokuwa za lazima kwani wametumia gharama ambazo hawakupaswa kutumia kulingana na hali mbaya ya kiuchumi ya timu.

“ TFF kwa msimu huu wa 2019/20 wangeacha tujiandae kwa msimu ujao, ligi ikiendelea ushindani utakuwa mdogo kwakuwa wachezaji wengi hawana nidhamu ya kufanya mazoezi watarudi wakiwa wazito ukichanganya na janga la Covid-19 hali ya uchumi imekuwa ngumu” , alisema Msilu

banner

Aliongeza kwa kusema kama TFF wataruhusu ligi iendelee basi watoe walau wiki mbili za kujipanga kila mchezo kutokana na hali mbaya kiuchumi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited