Home Makala Carlinhos Atua Rasmi Yanga

Carlinhos Atua Rasmi Yanga

by Sports Leo
0 comments

Fernandes Guimaraes ‘Carlinhos’ tayari ameshatua kwenye ardhi ya Tanzania akitokea Angola kwaajili ya kumalizana na mabosi wa Yanga Sc ili kuanza rasmi kuitumikia klabu hiyo yenye maskani yake Jangwani.

Kiungo huyo alikuwa anakipiga ndani ya Petro de Luanda ya nchini Angola ambapo alifanikiwa kutupia jumla ya mabao tisa na kutoa pasi tano za mabao.

Carlinhos alikubali kusaini dili la miaka miwili ndani ya Yanga Sc hivyo leo amekuja kukamilisha dili hilo ili kuanza mazoezi rasmi na wanajangwani hao ambao walishaanza maandalizi ya kuelekea wiki ya wananchi siku Jumapili Agosti,30.

banner

Yanga Sc ina malengo ya kuwatambulisha nyota wake wapya na wale ambao walikuwa na kikosi msimu uliopita katika siku hiyo ya Yanga Day ambapo pia inasadikika mwanamziki wa kizazi kipya,Harmonize ‘Konde Boy’atakuwepo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited