Home Makala Carlinhos Wa Yanga Atajwa na Kaze

Carlinhos Wa Yanga Atajwa na Kaze

by Dennis Msotwa
0 comments

Cedrik Kaze ambaye ni kocha mpya wa Yanga ameanza na safu ya ushambuliaji katika program zake za mazoezi kuhakikisha anapunguza ukame wa mabao katika kikosi chake.

Akianza na Carlos Fernandes ‘Carlinhos’ akimtaja kuwa anashindwa kuwapa pasi washambuliaji wenzake ambao ni Michael Sarpong,Yacouba Songne, Waziri Junior na Tuisila Kisinda.

Safu hiyo ya ushambuliaji wa Yanga mpaka sasa imefanikiwa kufunga mabao saba pekee ikiruhusu bao moja baada ya kucheza michezo mitano tangu kuanza kwa ligi kuu bara.

banner

Kaze alisema kuwa anaamini uwezo wa washambuliaji wake aliowakuta ingawa wanashindwa kuonesha umahili wao katika kufunga mabao kutokana na viungo wa timu hiyo kama Carlinhos kukosa mbinu za pamoja kuwapigia pasi za mwisho za kufunga mabao.

“Nimeanza kuiboresha safu ya ushambuliaji ili kuhakikisha natengeza muunganiko mzuri wa viungo na washambuliaji ambao kabla ya kuja kwangu haukuwepo “alisema Kaze

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited