Keulekea Mchezo wa siku ya Jumapili wa kombe la Shirikisho Barani Afrika dhidi ya Klabu ya Asec Mimosa Klabu ya Simba imetangaza kuwa itawakosa wachezaji wake Chris Mugalu ambaye amevunjika mkono, Kibu Denis Majeruhi ,Clatous Chama , Thadeo Lwanga majeruhi na Bernard Morrison aliye simamishwa
Kikosi hicho tayari kipo katika maandalizi ya mwisho ya mchezo huo huku nyota hao wakithibitishwa kukosekana katika mchezo huku ikitajwa kwamba tayari Kibu Dennis ameanza mazoezi taratibu na anatarajiwa kupatikana katika michezo ijayo.
Simba sc inakabiliwa na ratiba ngumu ya michuano ya kimataifa ikiwa na michezo takribani mitatu katika muda wa wiki mbili ambapo itacheza na Asec Mimosa siku ya Februari 13 nyumbani kisha itasafiri kuwavaa USGN februari 19 na baadae kucheza na Rs Berkane Februari 23.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.