Home Makala Che Malone Akalia Kuti Kavu Simba Sc

Che Malone Akalia Kuti Kavu Simba Sc

by Dennis Msotwa
0 comments
www.sportsleo.co.tz

Beki wa klabu ya Simba Sc Che Malone Akalia Kuti Kavu Simba Sc  kutokana na kuwa katika hatihati ya kusalia klabuni hapo kutokana na viongozi wa klabu hiyo kutoridhishwa na uwezo wake huku ikidaiwa kuwa kocha Fadlu Davis anahitaji beki mwingine kikosini humo.

Hata hivyo pia beki huyo upo hatua za mwisho za mazungumzo ya kujiunga na USM ALGER (USMA) ya Algeria kwenda kukipiga nchini humo baada ya mabosi wa klabu hiyo kuridhishwa na uwezo wa beki huyo.

Hadi sasa ni asilimia 90 Che Malone anaondoka ndani ya Simba Sports Club Kutokana na ofa hiyo ya Waalgeria kuwa nzito kiasi cha kuvutiwa nayo ikiwemo mshahara na fedha ya kusainia mkataba.

banner

Mbali na ofa hiyo,Che Malone Fondoh pia ana ofa ya MAS (Maghreb Fez) ya ligi kuu ya Morocco ila USM ALGER (USMA) ndio ambao wapo kwenye hatua nzuri za kumalizana na Che Malone hadi sasa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited