Home Makala Coastal Yabanwa Mbavu Na Yanga

Coastal Yabanwa Mbavu Na Yanga

by Sports Leo
0 comments

Yanga Sc imepata ushindi leo Octoba,3,2020 wa mabao 3-0 mbele ya Coastal Union katika mchezo wa ligi kuu bara uliofanyika uwanja wa Mkapa majira ya saa 1:00 usiku.

Kipenzi cha mashabiki wa klabu ya Yanga Sc, Carlos Carlinhos alianza kuzivamia nyavu za Coastal dakika ya 48 mara baada ya kutoka mapumziko ya kipindi cha kwanza na hapo aliandika bao la kwanza kwa klabu hiyo.

Bao la pili lilipachikwa na Haruna Niyonzima dakika ya 53 huku dakika ya 63 Yocouba Sogne alizikonga mioyo za mashabiki wao kwa kumalizia bao la tatu ambao ni la ushindi mkubwa na kuweza kunyakua alama tatu mbele ya Coastal Union.

banner

Coastal Union baada ya kufungwa walizidi kucheza kama kipindi cha kwanza wakizdi kutengeneza mashambulizi ambayo hayakuzaa matunda yoyote mbele ya wanajangwani hao.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited