Barcelona wapo tayari kusikiliza ofa kwa ajili ya Ousmane Dembele ikiwa vilabu vya Ligi kuu ya Uingereza Arsenal na Manchester United vimeonesha nia ya kutaka kumnasa winga huyo.
Kwasasa vilabu hivyo vinafanya uchunguzi kwanini Dembele amekuwa akiumia mara kwa mara .
Licha ya kwamba mara zote ujumbe wake umekuwa ni kutaka kuendelea kukupiga Camp Nou , Ousmane amekuwa akiulizia kuhusu maisha ndani ya miji mingine na hivi karibuni Hispania aliwasiliana na Anthony Martial .
Na kwa mujibu wa taarifa kutoka Hispania,Barca wapo tayari kumuuza winga huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 22 kwa dau la Pauni Milioni 43.