Home Makala Duchu Arejea Simba sc

Duchu Arejea Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imetangaza kumrejesha beki wa pembeni David Kameta maarufu kama Duchu ambaye alikua kwa mkopo katika klabu ya Mtibwa Sugar ambapo amesaini mkataba wa miaka mitatu kuendelea kusalia klabuni hapo.

Awali Duchu alisajiliwa na Simba sc akitokea Lipuli Fc lakini kutokana na changamoto ya namba alitolewa kwa mkopo katika klabu mbali mbali zikiwemo Geita Gold Fc na baadae akajiunga na Mtibwa Sugar ya manungu morogoro.

Simba sc imelazimika kumsajili beki huyo kuja kusaidiana na Shomari Kapombe upande wa kulia huku ikihamishia mlinzi wake Israel Mwenda upande wa kushoto kusaidiana na Mohamed Hussein hasa baada ya kumkosa beki waliyepanga kumsajili Yahaya Mbegu ambaye amejiunga na Singida Fountain Gate Fc.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited