Home Makala Epl Washirikisha Polisi Kutoa Mawazo

Epl Washirikisha Polisi Kutoa Mawazo

by Sports Leo
0 comments

Kundi la vilabu vya ligi kuu vimepanga kufanya mazungumzo na vikosi vyao vya polisi wiki hii kwa matumaini ya kuwa wazo la kutumia viwanja ambavyo ni tofauti na viwanja vyao (Neutral Venues) linaweza kubatilishwa.

Vilabu kadhaa vinaamini kuwa vikosi vyao vya Polisi  pamoja na kikundi vyao vya ushauri wa usalama, ambavyo huwa vinatoa ruhusa ya usalama na kuridhia kuchezwa kwa mechi vitathibitisha kuwa viko tayari kusimamia mechi za nyumbani ili tu kuwepo na mtindo wa nyumbani na ugenini na sio kutumia viwanja tofauti na vyao pindi ligi itakapo rejea .

Hata hivyo Premier League wanafikiria kubadili maamuzi ya vilabu kutumia viwanja tofauti na badala yake watumie viwanja vyao kama kawaida(usual stadium)ikiwa na maana kuwa kutakuwa na nyumbani na ugenini.

banner

Ikumbukwe kuwa vilabu vya Aston Villa, Brighton, na vingine vilivyopo chini ya msimamo wa ligi kuu England ni miongoni mwa vilabu vinavyopinga vikali wazo la kutumia viwanja tofauti na vyao (Neutral Venues) .

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited